Kwa uchungu mzito Mtangazaji, Zamaradi Mketema aomboleza kifo cha ghafla cha paka wake baada ya kushambuliwa na mbwa.
"Sijawahi kutegemea kama nitaumia hivi kwa kiumbe tofauti na mwanadamu, Paka wangu anaitwa HANNA, usiku sijui kitu gani kimemtuma atoke nje, kametokea dirishani akakutana na mbwa maana mbwa huwa tunawafungulia usiku tu wakamuumiza mno, na hii ni mara ya pili.
Mara ya kwanza alitokaga mbwa wakamshambulia bahati nzuri tuliwawahi akawa hoi lakini akapona kabisa akawa sawa, na akawa muoga kutoka ndani usiku sasa sijui kajisahau nini jamani katoka tena kilichomkuta this time hajapona, nimeumiaaaaa Mwan Kalikuwa karafiki kazuri sana, nikirudi tu nyumbani lazima anikimbilie, na kila ninapoenda anakuwa nyuma!!
"Na utakapokaa lazima kawe pembeni, na kuna muda kachokozi kwelikweli lakini ni usumbufu wenye raha ndani yake, Dah!! Nimeumia kwakweli," ameandika Zamaradi Mketema katika ukurasa wake wa Instagram.