Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Tundaman amemkumbuka aliyekuwa Meneja wa Kundi la Tip top Connection, Marehemu Abdu Bonge kwa kile alichodai kuwa amekufa na kundi hilo.
Alizungumza na waandishi wa Habari jana kwenye Iftari iliyoandaliwa na Chief Kiumbe jijini Dar es salaam, amesema kuwa ile Tip Top iliyokuwa na umoja enzi hizo kwa sasa haipo kwani kwa sasa wanafanya kazi kila mtu kivyake tofauti na zamani.
Tundaman amesema hata yeye licha ya kuwa kwenye kundi hilo lakini bado anasimamiwa na mtu mwingine kazi zake.
Miaka ya nyuma Tip Top Connection walishawahi kutamba na hits kibao kama Bado Tunapanda, Ridhiki, Goma la Manzese na nyingine kibao.
_______________________________________________________________________________________________
Kwa sasa unaweza kupata habari zetu zote sehemu moja kwa kupitia App yetu ya Bongo5. Pakua sasa kupitia Play Store kwa kubonyeza link hii – https://bit.ly/2J2Argw