Kuna njia nyingi za kupima Uwezo wa Akili ama IQ (Intellectual Quotient) kama inavyojulikana na wengi. Kwa lugha rahisi, uwezo wa akili ni kiashiria cha mtu cha kufikiri na kutatua matatizo.
Uwezo huu hupatikana kwa kugawanya alama ya umri wa kiakili ya mtu binafsi, inayopatikana kwa kusimamia jaribio la akili, kulingana na umri wao wa mpangilio na kuzidisha nambari hii kwa 100.
Tafiti ya hivi karibuni ya ‘Intelligence of Nations’ iliyoandaliwa na Richard Lynn na mwenzake David Becker, imezingatia sababu za kijenetiki na kimazingira katika tofauti hizi za viwango vya akili na athari zake katika nyanja mbalimbali, zikiwemo za kielimu, kiuchumi, kijamii na kidemografia.
Utafiti pia umeonesha kuwa viwango vya chini vya uzazi na viwango vya juu vya uhamiaji vitapunguza viwango vya akili katika nchi za Amerika ya Kaskazini, Japan na Ulaya huku vikitoa nafasi kwa China kuwa nchi yenye watu wenye akili zaidi, baada ya miaka 20.
Kwa kawaida, alama ya juu zaidi ya Uwezo wa Akili ni 130.