Msanii maarufu wa vichekesho nchini, TXDullah amesema kuwa si jambo baya kwa msanii mwenzake Harmonize kutumia sehemu ya maneno ambayo amekuwa akiyaibua na kuyafanya yawe maarufu kama "Ukilewa usichati".
Harmonize ametumia ametumia maneno ya "Ukilewa usichati" kwenye wimbo wake mpya na Rayvanny jambo ambalo TX amesema amefurahishwa nalo.
"Huwezi kumzuia msanii kutumia neno maana maneno siyo ya kwangu ni Lugha yetu ya Kiswahili. Kama hujasajili jina au kitu chochote, mtu akija akatumia wala hakuna shida, mimi najivunia harmonize kutumia maneno amaa misemo ambayo nimekuwa nikiibua na kuyafanya yawe mjini, huo ndiyo ubunifu wa msanii," amesema TXDullah.