Selena Gomez ambaye ni msanii na mfanyabiashara kutokea nchini marekani na mmoja kati ya wanawake wenye wafuasi wengi sana kwenye mitandao ya kijamii hivi majuzi ametoa sababu ya kushangaza na kuumiza pia kwa mashabiki zake kwamba hawezi kulala tena kitandani au chumbani kwake peke ake.
Selenagomez ana umri wa miaka 32 ambaye anasumbuliwa na ugonjwa aina ya 'bipolar dissorder' tatizo la kiakili ambalo husababisha huzuni na furaha zisizo za kawaida yanayojulikana kama maradhi ya hisia zinazobadilika
"nilikuwa natumia muda mwingi sana chumbani kwangu ambapo siwezi tena kulala hapo kwasababu ninahusisha pia na hali ya uwoga na ya kutisha" Selena gomez
Selenagomez alianza kusumbuliwa na ugonjwa huo mwaka 2020 ambapo septemba 2024 alisema kuwa hawezi kubeba mimba na kupata mtoto wake mwenyewe kutokana na maradhi yake.