Staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba maarufu wa AliKiba au King Kiba, kama kawaida yake, fundi wa kutunga na kuimba ameachia bonge moja la ngoma aliloipa jina la Mahaba.
Bosi huyo wa lebo ya Kings Music anayeshikilia rekodi ya mauzo makubwa ya albam Afrika Mashariki kupitia albam yake ya Cinderella ya mwaka 2006, ameiachia Mahaba leo Ijumaa, Februari 17, 2023.
Alikiba – Mahaba Lyrics
Sikuhizi hakuna mahaba yeh! Mahaba
Mapenzi ya mkataba mpaka kufa yamekwisha
Ni neema tuna hema mapenzi yanachosha yanafuja raha
Nafsi yangu inasema bora nimpende tu alonizaa
Uchungu wakulia daily
Mapenzi yalinifanya nisile
Sina kumbukumbu hile kwamba ulinikosha noo!
Uchungu wakulia daily
Mapenzi yalinifanya nisile
Sina kumbukumbu hile kwamba ulinitosha noo!
Mwenzako mi nilikufa nikazikwa nikaoza
Mapenzi yalinitesa yalinitupa nimefufuka yeh!
Mi nilikufa nikazikwa nikaoza
Mapenzi yalinitesa nimefufuka yeeh
Sikiliza kwanza we mdada we mdada
Mi sio mgeni yalishanikaba mapenzi yalinikausha
Natamani kua single ila nnaupwil unanikaba kooh
Mabinti wenye vifundo hao ndo mi wananitoa roho
Na siri tu ya jambo lile ni kama chakula lazima nile
Mi mbovu sana wa jambo lile na ufundi wa kutosha ooh
Na siri yake tu jambo lile ni kama chakula lazima nile
Mi mbovu sana wa jambo lile na ufundi wa kutosha ooh!
Mwenzako mi nilikufa nikazikwa nikaoza
Mapenzi yalinitesa yalinitupa nimefufuka yeh!
Mi nilikufa nikazikwa nikaoza
Mapenzi yalinitesa nimefufuka yeeh.