Ngoma ya Nana imefikisha views milioni 100 ndani ya miaka 9 , ikiwa ni project ya pili ya #DiamondPlatnumz ya kimataifa baada ya kufanya My Number One Remix ft @davido 2014, pia mwaka 2015 ilifanya vizuri sana kipindi hiko na kumuaminisha Simba #DiamondPlatnumz kuingia kwenye chart mbalimbali za muziki duniani, na kuchukua Tuzo ya #MTVMama kama Best perfomance of the year 2015.
Kwa Wimbo wa Nana kutimiza views milioni 100 unakuwa wimbo mmoja wapo Kati ya video ya 5 ya #Diamond kuwa na watazamaji zaidi ya milioni 100 kwenye mtandao wa Youtube, pia ni video ya pili ya au kolabo ya pili ya #Diamond na #Flavour kuwa na views zaidi ya milioni 100+,
Ngoma hii Inamfanya @diamondplatnumz , @burnaboygram na @wizkidy kuwa ndio wasanii wenye video nyingi zaidi kusini mwa jangwa la sahara Afrika zenye watazamaji zaidi ya milioni 100 kwenye mtandao wa Youtube,wote wakiwa na video 5 zenye watazamaji zaidi ya milioni 100+ kwenye Youtube Channel zao, Wakifatiwa na @davido mwenye video 4 zenye watazamaji zaidi ya milioni 100+.