Wakili wa Mtangazaji Masoud Kipanya, Alloyce Komba leo hii akizungumza na Waandishi wa habari ameweka wazi kuwa Mtangazaji Mwijaku inabidi atoe ushahisi kuwa Masoud Kipanya anajihusisha na biashara haramu kama anavyodai na akishindwa kutoa ushahidi inabidi atoe bilioni 5 kama fidia ya kumchafua Masoud Kipanya maana ameathirika kwa kiasi kikubwa mpaka kuna baadhi ya makampuni zimesitisha mikataba ya kufanya naye kazi.
Wakili wa Mtangazaji Masoud Kipanya, Alloyce Komba leo hii akizungumza na Waandishi wa habari ameweka wazi kuwa Mtangazaji Mwijaku inabidi atoe ushahisi kuwa Masoud Kipanya anajihusisha na biashara haramu kama anavyodai na akishindwa kutoa ushahidi inabidi atoe bilioni 5 kama fidia ya kumchafua Masoud Kipanya maana ameathirika kwa kiasi kikubwa mpaka kuna baadhi ya makampuni zimesitisha mikataba ya kufanya naye kazi. Mwijaku siku ya jana alitumia ukurasa wake wa Instagram kumshutumu Masoud Kipanya kuwa anafanya biashara haramu.