Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Mtoto wa miaka miwili afariki kwa kujipiga Risasi

Fdstfdfdf Mtoto wa miaka miwili afariki kwa kujipiga Risasi

Thu, 11 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Huko Douglas, Georgia nchini Marekani, mtoto wa miaka 2 aliyefahamika kwa jina la Nakyzi Odums, amefariki dunia baada ya kujipiga risasi kimakosa kwa kutumia bunduki ya wazazi wake iliyosahaulika kwenye gari wakati wazazi wake wakiwa dukani siku ya Julai 3.

Mashuhuda wamesema wazazi hao wakiwa dukani walisikia mlio wa risasi na kukimbilia kwenye gari ambapo walimkuta mtoto huyo akiwa na jeraha kubwa kifuani kwake.

Mtoto huyo alikimbizwa hospitali ya karibu kwa ajili ya kuokoa maisha yake lakini alifariki siku ya Jumamosi ya Julai 6.

Haijajulikana bado kama wazazi hao watakabiliwa na mashtaka yoyote kuhusiana na kifo cha mtoto huyo.

Mkuu wa Polisi wa Douglas. Brannen Pruette aliliambia gazeti la The Independent:

“Unaruhusiwa kuwa na bunduki ndani ya gari, lakini kunapokuwa na mtoto unapaswa kuhakikisha kuwa bunduki hiyo iko sehemu salama ili mtoto asiione.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live