Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

'Mama yangu aliambiwa nitafariki dunia ndani ya wiki mbili'

Waridii  03 At 18.jpeg 'Mama yangu aliambiwa nitafariki dunia ndani ya wiki mbili'

Wed, 3 Jul 2024 Chanzo: BBC Swahili

Ulikuwa ni usiku wa kawaida kama zilivyo siku nyingine, kitandani binti wa umri wa miaka mitano ambaye hakuwa na ulemavu wowote ule akiwa amelala, alishtuka ghafla na kuhisi kwenda msalani.

Jambo la kushangaza, Zena Akuwa, alishindwa kusimama siku hiyo na kuamua kuomba msaada kutoka kwa mama yake.

“Nilimuita mama yangu ili aniinue lakini kwa sababu mimi ni mtoto wa mwisho mama aliniambia acha kudeka nenda msalani, ile nasimama tu nikaanguka chini”. Anasema Zena.

‘’Nilipoteza uwezo wa kusimama,miguu yangu ilikuwa inalegea kabisa. Kila mtu alishangaa na hata mimi mwenyewe sikuelewa nini kinanitokea, nilikuwa nikisimama sisikii kama nina miguu’’anaeleza zaidi.

Wazazi walipigwa na butwaa na kuamua kumpelekea hospitali na kumhangaikia kwa kila hali ili kupata ufumbuzi wa hali iliyompata.

‘Nilipoteza fahamu tukiwa Mlimba Morogoro, nilipoamka nilijikuta tayari nipo hospitali ya taifa Muhimbili Dar es Salaam’.

Baada ya vipimo vya wataalam, tatizo la Zena halikuweza kubainika chanzo chake kwani hali yake ilikuwa ikibadilikabadilika na ilifika mahali alipoteza uwezo wa kuona.

Hali ya Zena ilifika wakati hata madaktari walikata tamaa iwapo angeendelea kuishi. “Kuna daktari mmoja alimwambia mama inawezekana ndani ya wiki moja au mbili mtoto wako akafariki dunia kwa sababu hata sisi hili tatizo tunashindwa kuelewa ni kitu gani”.

‘’Mama yangu alihangaika sana ili kupata ufumbuzi wa tatizo langu. Alihangaika hospitali, misikitini makanisani ilimradi tu nipate uponyaji”, anasimulia Zena.

Na hapo ndipo safari yake ya ulemavu ilipoanzia, akawa mtu wa kubebwa kila mahali.

Alipoteza matumaini ya kuishi, alikata tamaa na hakuwa akielewa chochote kinachoendelea. Kwa msaada wa madaktari alipata tena uwezo wa kuona.

‘”Nilifumbua macho na fahamu zilirudi na kitu cha kwanza nilimwambia mama yangu naomba chakula. Huenda ndiyo maana napenda sana kupika’’, anasema Zena huku akitabasamu.

Chanzo: BBC Swahili