Menu ›
Burudani
Mon, 18 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mama mzazi wa supastaa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz aitwaye Sanura Kasimu maarufu kama Mama Dangote amesema kuwa mwanaye huyo ana chembechembe za asili ya Congo DR ndiyo maana anafanya vizuri kwenye muziki wake.
Ikumbukwe kuwa, Wakongomani wanatamba sana kwenye tasnia ya muziki na wamekuwa wakifanya vizuri ndani na nje ya Bara la Afrika.
"Mwanangu Naseeb (Diamond Platnumz) kwa upande mkubwa yeye ni mkongo na ndio maana hata hii nyimbo aliomshirikisha mjomba ake Koffi Olomide imekubalika Sana na wakongo kwa sababu ni mtoto wao," amesema Mama Dangote.
Unakubaliana na hilo?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: