Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Maajabu: Waliofanya utafiti wa kifo ili wasife

Qin Shi Huang.png Maajabu: Waliofanya utafiti wa kifo ili wasife

Mon, 27 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ukiitazama hali ya ulimwengu wa leo, unaweza kushangaa au kufurahia kwa kufikiri kwamba baadhi ya Watawala watangulizi hawakuwa makini au walikuwa mashujaa au unaweza enda mbali zaidi ukawalaumu au kuwapongeza, kutokana na vile unavyoiweka tafsiri yako katika kutazama mambo ya kale.

Hali hii siyo jambo jipya kwani tayari wengi waliotangulia nao walishangaa au kufurahia kama wewe kutokana na hisia zao, mfano kuna watu wamekuwa wakiwavumilia watawala wao ambao walipoteza umakini na kufanya mambo yasiyofaa ama ya kupendeza yaliyoacha historia, kwani baadhi yao walichekesha, wengine wakaogopwa kwa ukatili wao.

Hapa nakuletea matukio machache ambayo wewe nawe utatoa tafsiri yako kulingana na kile kilichoandikwa na Wazee wetu hawa wakongwe walioacha alama katika maisha ya Dunia kutokana na haiba yao ya uongozi na mapokeo ya wale waliowaongoza, najua hukuwepo lakini utajifunza kitu.

1. Qin Shi Huang akichunguza kifo

Qin Shi Huang alikuwa mtawala ambaye aliamini mambo yake yeye mwenyewe. Aliingia madarakani kama mfalme wa kwanza wa China iliyoungana katika karne ya 3 KK, ambapo mara tu alipopata mamlaka, alihangaikia sana kwani alikuwa na maadui wengi na kwa miaka mingi alikabiliana na majaribio kadhaa ya kutaka kuuawa.

Wazo la kwamba kifo ndicho pekee ambacho kingeweza kumtenganisha yeye na madaraka, kilimfanya apoteze fikra kwani alikuwa na hamu ya kupata njia ya kutokufa hivyo aliwasiliana na madaktari ambao walimwekea utaratibu mzuri wa kudumisha uhai wake.

Alishindwa masharti hapo akaanza kumeza vidonge vilivyojaa zebaki lakini dawa hizo zilikuwa na athari kwani afya yake ilidhoofika na uwezo wake wa kufikiri ulipungua hivyo ikambidi kuwaagiza wasaidizi wake kwenda kudadisi wakuu wa ‘Visiwa vya Wasiokufa’ kutafuta dawa ya kichawi ambayo ingemruhusu kuishi milele.

Na kwa kuogopa watu waovu, Qin Shi Huang alikuwa na mfumo tata wa maisha ya kujificha kwani alitengeneza mfumo wa vichuguu vilivyojengwa, ambavyo viliunganisha majumba yake yapatayo 200 ili hata atakapovamiwa basi adui asiweze kufanikiwa lengo lake kirahisi, lakini hata hivyo aliaga dunia miaka ya 210 BC akiwa na umri wa miaka 49.

Huang anakumbukwa zaidi kwa utafiti wake huo wa kutokufa, kumbukumbu yake ikisalia katika kaburi lake alilozikwa pamoja na jeshi lake la askari wa terracotta, ambao kwa pamoja walikula yamini wakikusudia kuwa jeshi lisiloweza kufa, wakiapa kumlinda mfalme wao (Qin Shi Huang), aliyedaiwa kuwa naye hawezi kufa, wakipanga kutawala milele na milele.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live