Rapa Killer Mike ameendelea kugonga vichwa vya habari baada ya kushinda tuzo ya albamu bora ya mwaka kwenye tuzo za BET 2024 nchini Marekani.
Mike alishika vichwa vya habari mapema mwezi Februari mwaka huu aliposhinda tuzo ya Grammy na kukamatwa na polisi baada ya kudaiwa kuleta vurugu kwenye hafla ya tuzo hizo.
Rapa huyo huenda akakwepa mashtaka kuhusu ugomvi wa kimwili uliosababisha kukamatwa kwake kwenye tuzo za Grammys baada ya kumaliza adhabu yake ya kufanya huduma za kijamii.
"Nasema asante...nimejinyenyekeza kupata tuzo hii. Asanteni kwa kuniona, kuniamini na kuniheshimu kwa njia hii," Mike amesema baada ya kushinda tuzo hiyo.