Menu ›
Burudani
Wed, 21 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Mara baada ya kuonekana wakiwa pamoja na wasanii wa WCB, Director Nisher amejibu iwapo kuna kazi zinakuja kati yao.
Nisher ameiambia Bongo5 bado ni mapema kuzungumzia hilo kwa sasa ila kuna kazi nyingi zinakuja.
“Hiyo siwezi kusema isipokuwa kitu ambacho nakumbuka nilikuwa na show nilikutana na watu kibao kama kina Rich Mavoko, Harmonize, Ray C, AY na Fid Q pia, kwa hiyo kuhusiana na kazi zinazokuja siwezi kuongelea sana japokuwa kuna kazi kibao zinakuja,” amesema Nisher.
Video ya Dogo Janja ‘Wayu Wayu’ ambayo inafanya vizuri kwa sasa ni moja video ambazo Nisher kwa mwaka huu.
Chanzo: bongo5.com