Dulla Makabila juzi Disemba 19 ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la "Pita huku".
Wimbo huo wa Dulla Makabila umepokelewa vyema sana mtaani huku ukifanya vyema You Tube kwani ndio wimbo unaoongoza mpaka sasa katika trending.
Sasa baada ya kutoa wimbo huo Dulla Makabila amepokea wito kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambao ndio walezi wa muziki nchini.
Wito huo ullibua hisia tofauti kwa wapenzi wa muziki waiohoji kama kisa ni wimbo huo hakuna baya lililofanyika na msanii ametumia ubunifu wa hali ya juu katika uandishi wa nyimbo hiyo.
Sasa Dulla ameitikia wito na hiki ndicho kilichozungumzwa katika kikao na BASATA.