Katika hali isiyo ya kawaida kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Laiza, mkazi wa mtaa wa Kivukoni Kata ya Kalangalala Halmashauri ya Mji wa Geita, amekutwa na chupa nyingi zilizojaa mkojo chumbani kwake ambazo zinatoa harufu kali inayowaathiri majirani wa eneo hilo.
Akizungumzia tukio hilo mama mwenye nyumba hiyo pamoja na majirani zake wamesema wilikuwa wanasikia harufu mbaya kwa muda mrefu ikitokea katika chumba chake huku wakidhani pengine kuna mtu amefariki, kutokana na mwenye chumba kutoonekana muda mrefu.
Baada ya askari kujulishwa kwaajili ya upekuzi ndipo walipovunja mlango na kukuta hali hiyo.