Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Haya ndio mambo ya kuzingatia unapotaka kununua simu (+Video)

Video Archive
Tue, 23 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kwenye ulimwengu huu wa teknolojia zipo aina nyingi za simu, kutokana na uwepo wa kampuni nyingi za kutengenea bidhaa hizo.

Lakini ukiwa kama mtumiaji na mteja wa vifaa hivyo ni muhimu kuzingatia haya unapoenda kununua simu mpya. Kwanza hakikisha una bajeti ya kutosha kununua simu unayotaka.

Pili katika manunuzi hayo zingatia sifa za kiufundi za simu kama vile 'Processor', hii inahusiana na kasi ya simu kwenye utendaji kazi wake.

'RAM' hii inasaidia katika utendaji wa 'multitasking', kufanya kazi zaidi ya moja kwenye simu. Kisha hakikisha ina nafasi ya kutosha kwa matumizi yako.

Aidha ikiwa unataka picha bora, angalia megapixels na ubora wa kamera. Usisahau ubora wa betri chunguza kiwango cha mAh kinachoweza kukaa na chaji kwa muda mrefu.

Mfumo wa uendeshaji angalia kama ni Android, iOS, au nyingine na toleo lake. Zingatia ukubwa na ubora wa skrini (OLED, LCD, nk.) ni muhimu kwa mtumiaji.

Angalia kama inauwezo wa 4G/5G, Wi-Fi, na Bluetooth. Hakikisha simu ina muonekano mzuri na ni imara. Mwisho zingatia ukubwa na uzito, chagua simu ambayo ni rahisi kushika na kubeba. .

Chanzo: www.tanzaniaweb.live