Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hali ya mtunzi wa wimbo wa ‘Tanzania yetu ndio nchi ya furaha’ yatia matumaini

Video Archive
Mon, 5 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) leo Jumanne Februari 27, 2018 limemtembelea mtunzi wa wimbo uliovuma zaidi miaka ya nyuma wa ‘Tanzania yetu ndio nchi ya furaha’, Mzee Stephen Hizza ambaye anasumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya tezi dume.

?Katibu Mtendaji Godfrey Mngereza (Kulia) akimjulia hali Mzee Stephen Hizza aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Mzee Hizza amelazwa wiki chache zilizopita katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wodi ya Kibasila Chumba Na.16 ameonekana afya yake kuendelea vyema tofauti na kipindi cha nyuma kama ilivyoripotiwa awali na vyombo vya habari.

Wimbo wa ‘Tanzania yetu ndio nchi ya furaha’ uliimbwa na Bendi ya ‘ Atomic Jazz Band’ miaka ya 19 70’s ikiongozwa na John Kijiko. Jikumbushe wimbo huo hapa chini

Chanzo: bongo5.com