Menu ›
Burudani
Mon, 5 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) leo Jumanne Februari 27, 2018 limemtembelea mtunzi wa wimbo uliovuma zaidi miaka ya nyuma wa ‘Tanzania yetu ndio nchi ya furaha’, Mzee Stephen Hizza ambaye anasumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya tezi dume.
Mzee Hizza amelazwa wiki chache zilizopita katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wodi ya Kibasila Chumba Na.16 ameonekana afya yake kuendelea vyema tofauti na kipindi cha nyuma kama ilivyoripotiwa awali na vyombo vya habari.
Wimbo wa ‘Tanzania yetu ndio nchi ya furaha’ uliimbwa na Bendi ya ‘ Atomic Jazz Band’ miaka ya 19 70’s ikiongozwa na John Kijiko. Jikumbushe wimbo huo hapa chini
Chanzo: bongo5.com