Menu ›
Burudani
Wed, 15 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Siku chache baada ya msanii Gnako Warawara kuwachimba mkwara wasanii wenzake wa kundi la Weusi kwamba kama hawataachia wimbo mpya 'soon', basi atavujisha wimbo wao, leo ameibuka na jipya.
Kupitia akaunti yake ya mtandao wa X (zamani Twitter), G Nako ameandika:
"Kwa hiyo kwa miaka yote hiyo hamnaga kundi bora tena kama weusi East Africa? Kama lipo mtanambia..."
Wafuasi wake katika mtandao huo, wametiririka kwenye 'comments', kila mmoja akisema lake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live