Rich Mitindo ambaye ni mfanyabiashara ambaye pia ni mpenzi na mzazi mwenzake na supastaa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper ametoa exclusive kutangaza rasmi tarehe ya ndoa yao.
Akihojiwa kupitia eNewz ya East Africa TV, Rich mitindo ambaye amezaa mtoto mmoja na Wolper na wanategemea mtoto wa pili hivi karibuni, amesema;
“Sina kitu ambacho sipendi Wolper afanye kwa sababu tunaambiwa ‘mpende mtu kutokana na mapungufu yake’. Kwa hiyo leo nikisemasimpendi kutokana na mapungufu yake nitakuwa mnafiki, nampenda kwa kila kitu.
“Kwa sasa tunatarajia mtoto wa pili, ndoa yetu itakuwa tarehe 19, mwezi Novemba, 2022, hiyo ni exclusive nimekupa,” amesema Rich Mitindo.