Menu ›
Burudani
Thu, 14 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Supastaa wa Muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amewachana waliomsema vibaya wakati alivyoachia wimbo wake wa 'Shu'.
Hii ni baada ya mapokeo mazuri ya wimbo huo ambao video yake imefikisha watazamaji milioni 7.4 tangu aiachie miezi miwili iliyopita huku akisema kuwa anapowaza ni ngumu mtu mwingine kufika.
"Hii Shu imejua kunidhalilishia watu, jamani mnapoona natoa ngoma punguzeni uchambuzi ushuzi maana niwazapo hamuwezi fika.
"Na sijawa tu msanii kwa bahati mbaya, ni Mwenyezi Mungu alinijaalia niwe hivyo,kuwa anavyonionesha ambavyo akili yako haiwezi kamwe viona," amesema Diamond.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: