Ebwana hii inaweza kuwa ni stori kubwa katika kiwanda cha Muziki Bongo Flavour, Baada ya Msanii anaefanya vyema kwenye Game la Bongo Flavour, Jay Melody kuandaa Shoo yake katika ukumbi wa Ware House Masaki usiku wa tarehe 20 Julai.
Sasa kubwa ni kuwa siku chache zilizopita Diamond Platnumz aliahidi kuja kumpa Sapoti Jay Melody katika Shoo hiyo, Guess Whaaaat? mpinzani wa karibu wa CEO huyo wa Lebo ya Wasafi, Ally Kiba “King Kiba” nae ametusanua kuwa atatokea katika show hiyo kuja kumpa sapoti Jay Melody..!
Kwa Maana hiyo wakali wawili wenye upinzani wa hali ya juu kwenye Game ya Bongo Fleva wataoneka Ware house Masaki leo Julai 20, we unakosaje?
Acha inyeshe, tuone panapovujaaaaa