Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Binti mfalme wa Dubai atangaza kumtalaki mume wake kupitia Instagram

Binti Mfalme Wa Dubai Atangaza Kumtalaki Mume Wake Kupitia Instagram.png Binti mfalme wa Dubai atangaza kumtalaki mume wake kupitia Instagram

Thu, 18 Jul 2024 Chanzo: Bbc

Binti wa mtawala wa Dubai ametangaza kumtalaki mume wake kupitia mtandao ya kijamii.

Ujumbe kutoka kwa akaunti ya Instagram iliyothibitishwa ya Sheikha Mahra bint Mohammed bin Rashid Al Maktoum ulisema anakatisha ndoa yake kwa kuandika: "Mimi natangaza talaka yetu."

BBC imewasiliana na maafisa nchini humo ili kupata ufafanuzi kuhusu suala hilo.

Hadi kufikia sasa, sio mume wake Sheikha Mahra, Sheikh Mana bin Mohammed bin Rashid bin Mana Al Maktoum, wala baba yake, ambaye ametoa maoni kuhusu suala hilo kwa umma.

Ujumbe huo, ambao ulianza kwa kusema "Mume wangu Mpendwa", ulihitimishwa na maneno - "Ninakupa talaka, ninakupa talaka, na ninakupa talaka," ukionekana kutumia desturi ya Kiislamu inayojulikana kama talaka tatu.

Kitendo hicho kimepigwa marufuku katika nchi nyingi, lakini kwa kawaida huwaruhusu waume kuwataliki wake zao haraka kwa kusema “Ninakupa talaka” mara tatu.

"Kila la kheri. Mke wako wa zamani," ujumbe huo wa kwenye Instagram uliandikwa.

Picha zote za mume wa Sheikha Mahra zinaonekana kuwa zimefutwa kwenye akaunti yake.

Vile vile, akaunti ya Sheikh Mana inaonyesha picha za mke wake zimefutwa.

Wenzi hao walioana mnamo Aprili 2023 katika sherehe ya kifahari, na mtoto wao wa kwanza alizaliwa miezi miwili iliyopita.

Baadhi ya maoni kutoka kwa watumiaji wa Instagram wanakisia kuwa akaunti ya Sheikha Mahra inaweza kuwa imedukuliwa lakini hakujakuwa na dalili au usemi rasmi juu ya hilo.

Wakati ujumbe huo wa kumtalaki mume wake unaonekana ulionyesha kuwa umekuwepo kwa siku moja.

Serikali ya Dubai na Ubalozi wa UAE mjini London hawakujibu mara moja maombi ya kupata maoni yao.

Chanzo: Bbc