Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Albamu ya Chin Bees ‘Ladha’ kutolewa bure (+video)

Video Archive
Thu, 8 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Baada ya kuachia albamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Ladha, msanii wa muziki Bongo, Chin Bess ameweka wazi kuwa albamu hiyo itapatikana bure kabisa kwa njia zote zile.



Chin Bees amesema sababu ya kufanya hivyo ni kwamba mwaka jana mashabiki wake walifanikisha ngoma yake ya Kababaye kufika mbali, hivyo albamu hiyo ni zawadi kwao.

“Kwa hiyo hii ni kama zawadi kwa mashabiki wangu, nimewaletea hii wafurahi inapatikana bure kabisa, unaweza ku-downlod mtandaoni ni bure kabisa, hivyo narudisha upendo kwao,” amesema.

Chin Bees ni msanii wa kwanza wa Bongo Flava kutoka albamu kwa mwaka huu mara baada ya Vanessa Mdee kufanya hivyo mwishoni mwa mwaka jana. Pia mwaka huu wasanii kama Wakazi na Diamond wanatarajiwa kutoa albamu.

Chanzo: bongo5.com