Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

TV

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakamatwa kwa kuiba bunduki kituo cha polisi

BUNDUKI Kujiuaaa Wakamatwa kwa kuiba bunduki kituo cha polisi

Wed, 16 Oct 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Katika tukio la kushangaza lililotokea Kamukunji, Nairobi, watu wawili wamekamatwa kwa kuiba bunduki ya afisa wa polisi, Inspekta Fredrick Muzungu, iliyopotea miezi miwili iliyopita muda mfupi baada ya kuegesha gari katika kituo cha polisi cha Jogoo Road.

Jambo la kustaajabisha ni kwamba gari hilo halikuonesha dalili zozote za kuvunjwa, jambo lililosababisha taharuki kuhusu ni kwa namna gani wahalifu waliweza kuipata silaha hiyo yenye risasi 15 pamoja na pingu, simu aina ya Motorola, na simu nyingine ndogo.

Baada ya tukio hilo, Afisa wa Upelelezi wa Eneo (DCIO) aliamuru kukamatwa kwa Inspekta Muzungu ili kusaidia kwenye uchunguzi wa sakata hilo, ambapo bunduki hiyo haikupatikana hadi watoto waliokuwa wakicheza mpira karibu na jengo la Railway House walipoikuta imefichwa chini ya kibanda, umbali wa mita 900 kutoka kituo cha polisi.

Uchunguzi zaidi ulipofanyika, wananchi walitoa taarifa muhimu kuhusu tukio hilo, wakidai kuwa waliona watu wawili wakiweka kitu kwenye kibanda hicho na baada ya upelelezi waliweza kuwakamata watu wawili Alex Odhiambo na Amos Owino kwa kuhusika na tukio hilo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live