Menu ›
Biashara
Tue, 23 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Huu ni mradi unaomilikiwa na wawekezaji wa kitanzania ambapo wanafanya uchimbaji na uchenjuaji wa madini ya dhahabu katika eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime mkoani Mara.
Mradi huu wenye thamani ya dola za Marekani milioni 10 (shilingi bilioni 27), leo Julai 22, 2024, umetembelewa na maafisa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
Ziara hii ni mwendelezo wa kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani inayoendelea Kanda ya Ziwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live