Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO: Serikali ya Tanzania yasaini mkataba ununuzi wa Bombardier

Video Archive
Mon, 21 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wakala wa Ndege za Serikali ya Tanzania (TGFA) na kampuni ya kutengeneza ndege ya Canada-'De Havilland' wamesaini mkataba wa ununuzi wa ndege moja aina ya Bombardier Q400.

Mkataba huo umesainiwa leo Jumamosi Oktoba 19, 2019 lengo likiwa ni kuimarisha na kuboresha utoaji huduma za usafiri wa anga nchini kupitia Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).

Mtendaji mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali, Dk Benjamin Ndimila amesema ndege hiyo itakua na uwezo wa kutua hata kwenye viwanja vya vumbi.

"Ndege hii mpya inatarajiwa kufika nchini kati ya  Juni au Julai 2019, " amesema Dk Benjamin licha ya kutoeleza imenunuliwa kiasi gani.

Tangu 2016 Serikali imekuwa ikinunua ndege na hivi karibuni

inatarajia kuongeza ndege nyingine tatu.

Pia Soma

Advertisement
Makamu wa Rais wa mauzo wa kampuni hiyo, Sameer Adam ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kununua ndege kwa lengo la kuboresha na kuimarisha huduma za usafiri wa anga.

"Hongera nyingi kwa Tanzania kwa hatua hii nyingine ya kuongeza ndege mpya, " amesema Sameer.

Naye mkurugenzi mkuu wa ATCL,  Ladislaus Matindi amesema, “baada ya ununuzi wa ndege hii mpya kukamilika tutakuwa na ndege tano ndogo ambazo zitatumika kutoa huduma za usafiri wa anga nchini na nchi za jirani.”

Amesema shirika hilo litaendelea kuboresha huduma zake kwa kuzifanyia kazi kero wanazokumbana nazo wateja zikiwamo kuchelewa na kusitishwa kwa safari za ndege.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz