Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO: Serikali ya Tanzania yaeleza inavyowekeza kwenye elimu

Video Archive
Fri, 20 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Waziri wa Elimu nchini Tanzania, Profesa Joyce Ndalichako ameeleza namna Serikali ilivyowekeza katika ya elimu  kuhakikisha inafikia azma ya kuwa na wananchi walioelimika, wenye maarifa, stadi za maisha na mtazamo chanya.

Ameeleza hayo leo Alhamisi Septemba 19, 2019 katika mjadala wa vijana na elimu katika jukwaa maalum maarufu kama Mwananchi Jukwaa la Fikra linalofanyika katika ukumbi wa Kisenga, jijini Dar es Salaam.

Profesa Ndalichako aliyeanza kwa kuipongeza kampuni ya Mwananchi Communication Ltd (MCL) kwa kuandaa jukwaa hilo leo ikiwa ni mara ya tano, amesema linaisaidia Serikali kusikia masuala ya wananchi.

Amebainisha kuwa kuanzia Januari 2016 hadi Agosti, 2019  Serikali imetumia zaidi ya Sh900 bilioni  kugharamia elimu bure ambayo imekuwa na mwamko mkubwa na kusababisha changamoto ya vyumba vya madarasa.

Amesema Serikali imejaribu kupambana na changamoto hiyo, imeshatumia zaidi ya Sh300 bilioni kuboresha miundombinu ikiwemo shule mbalimbali zikiwemo kongwe 62 kati ya 88 zilizopo.

“Tumejenga madarasa 2876, mabweni  533, nyumba za walimu na miundombinu mingine ya shule. Tangu Serikali hii iingie madarakani tumeweza kutoa mikopo ya zaidi ya Sh1 trilioni kwa wanafunzi wa elimu ya juu,” amesema Profesa Ndalichako.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Mbali na hilo, Profesa Ndalichako amesema Serikali imeboresha vyuo vya ufundi stadi ikiwemo kujenga vyuo na kuvikarabati  katika mikoa mbalimbali nchini kikiwemo cha Kilimo cha Sokoine (SUA).

Chanzo: mwananchi.co.tz