Menu ›
Biashara
Tue, 2 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amesema maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Sabasaba yanatarajia kutengeneza ajira za muda zipatazo 11,712.
Kigahe amesema hayo wakati alipotembelea na kukagua maandalizi ya ufunguzi rasmi wa maonesho hayo yanayoendelea kwenye Viwanja vya Julius Nyerere mkoani Dar es Salaam.
Amesema maonesho ya mwaka huu yatakuwa ya aina yake, yakijikita katika kuonesha teknolojia za hali ya juu, ubunifu na matumizi ya akili mnemba (AI).
Chanzo: www.tanzaniaweb.live