Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nyama ya maabara sasa ruksa

Nyama Maabara BM 1200 80 Nyama ya maabara sasa ruksa

Fri, 19 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Uingereza imekuwa Nchi ya kwanza Barani Ulaya kuidhinisha nyama iliyotengenezwa maabara na hivyo kufungua njia kwa kuku wa kukuzwa maabara kuanza kuuzwa katika maduka ya wanyama wa kufugwa mapema mwaka huu.

Uanzishaji wa kampuni inayozalisha nyama hizo ya “Meatly” Nchini Uingereza umeidhinishwa na Wadhibiti ubora wa Uingereza kwa nyama yake inayokuzwa kwenye maabara ili itumike katika chakula cha mifugo.

Uingereza sasa itakuwa Nchi ya kwanza ya Ulaya ambayo chakula cha wanyama kilichokuzwa kwenye maabara kinapatikana kwa Watu kununua, nyama hizo ni kwa ajili ya chakula cha wanyama kama vile mbwa, paka n.k.

Owen Ensor, Mtendaji Mkuu na Mwanzilishi mwenza wa Meatly, amesema hii imetokana na msukumo kutoka kwa Wadhibiti na Serikali kutetea uvumbuzi wa chakula na kuharakisha michakato ya kuidhinisha baada ya Brexit na Uingereza kuchukua “faida yake ni kubwa.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live