HoteI ya kitalii ya Ngurdoto Mountain Lodge yenye hadhi ya nyota tano iliyopo Arumeru mkoani Arusha, imegeuzwa hosteli ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) baada ya kufungwa kwa siku kadhaa kutokana na ukosefu wa wateja, baada watalii kutoka nje kupungua kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya corona, Covid-19 duniani.
HoteI ya kitalii ya Ngurdoto Mountain Lodge yenye hadhi ya nyota tano iliyopo Arumeru mkoani Arusha, imegeuzwa hosteli ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) baada ya kufungwa kwa siku kadhaa kutokana na ukosefu wa wateja, baada watalii kutoka nje kupungua kutokana na janga la ugonjwa wa virusi vya corona, Covid-19 duniani. Mkuu wa chuo hicho, Prof. Eliamani Sedoyeka, amethibitisha chuo chake kuingia mkataba na Kampuni ya Landmark inayoisimamia hoteli hiyo na kwamba wamepata nafasi ya kutosha malazi ya wanafunzi.