Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bolt yamteua Dimmy Kanyankole kuwa Meneja mpya wa Tanzania

Tanzaniaweb Bolt Yamteua Dimmy Kanyankole Kuwa Meneja Mpya Wa Tanzania

Fri, 28 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kampuni inayoongoza kwa huduma za usafirishaji Tanzania na Barani Afrika, inafuraha kuwataarifu kuhusu uteuzi wa Bw.Dimmy Kanyankole kuwa Meneja mpya wa Bolt nchini Tanzania. Hatua hii ya kimkakati ni sehemu ya dhamira inayoendelea ya kampuni katika kuimarisha shughuli zake na uzoefu wa wateja katika kanda.

Dimmy ni kiongozi atakayesimamia mapato yatokanayo na biashara na kufuatilia rekodi ya maendeleo ya biashara, utendaji wa masoko, usambazaji, uendeshaji wa kibiashara na usimamizi wa timu.

Analeta uzoefu mwingi kwa rekodi iliyothibitishwa kwake kwa kufanya kazi na makampuni yanayoongoza ya Pan African renewable energy na Fintech kama vile Engie and Cellulant. Dimmy ameonyesha kuwa kiongozi wa kipekee na mwenye uelewa wa kina wa mienendo ya soko, na kumfanya kuwa anafaa kikamilifu kwa jukumu hili muhimu.

Kabla ya kujiunga na Bolt, Dimmy alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Uuzaji wa Rejareja wa Cellulant, kampuni inayoongoza Afrika ya Fintech. Alikuwa akiongoza mauzo ya rejareja yanayohusisha na ukuaji wa jumla wa bidhaa katika masoko 6 ya Afrika (Kenya, Uganda, Tanzania, Ghana, Nigeria & Zambia).

Katika kazi hiyo, alikuwa anawezesha wauzaji (SME), ukuaji wa bidhaa na ukuaji wa mapato kwa ujumla. Kabla ya hapo, aliwahi kuwa Mkuu wa Kitengo cha Uanzishaji(Activations) na alikuwa akiendesha bidhaa za Billpay & Checkout, ambapo aliwajibika kwa mamia ya wafanyabiashara wa kimataifa na wa ndani kote Afrika. Pia alisaidia Engie (zamani Mobisol) kuimarisha nafasi yao kama kampuni inayoongoza ya nishati mbadala katika kanda.

Caroline Wanjihia, Mkurugenzi wa Masoko Bolt Kanda ya Afrika na Kimataifa alisema: “Tunafuraha kumkaribisha Dimmy kwenye timu yetu. Uzoefu wake mkubwa na mitazamo yake ya kimaono utasaidia sana katika kuendesha dhamira yetu ya kutoa suluhisho za usafiri zilizo salama, za kutegemewa na zinazofaa kwa watu wa Tanzania, tuna imani kwamba ataongoza shughuli zetu kwa mtazamo mpya."

Chini ya uongozi wa Dimmy, Bolt inalenga kuimarisha zaidi uwepo wake nchini Tanzania, kwa kuzingatia uvumbuzi, usalama, na kuridhika kwa wateja. Uteuzi wake unakuja wakati muhimu huku kampuni hiyo ikiendelea kuzindua mipango kadhaa mipya iliyobuniwa kuboresha utoaji wa huduma na kupanua wigo wake kote nchini.

Hivi karibuni, Bolt Tanzania ilizindua kituo chake cha huduma na mafunzo kwa Madereva katika juhudi za kuimarisha uhusiano wa madereva na kushughulikia matarajio yao katika kushughulikia matatizo yao.

Dimmy Kanyankole, Meneja wa Bolt Tanzania alisema: “Ninayo furaha kujiunga na Bolt kama Meneja mpya wa Tanzania. Nitajitolea kwa dhati kwa uvumbuzi na kuridhika kwa wateja, ninafurahi kuiongoza timu yetu iliyojitolea katika kuboresha uzoefu wa usafiri kwa watanzania wote.

Lengo letu litakuwa katika kupanua huduma zetu, kuhakikisha usalama kutegemewa, na kukuza ushirikiano thabiti ndani ya jamii kwa pamoja, tutaendelea kukuza ukuaji na kutoa thamani ya kipekee kwa abiria na madereva wetu kote nchini."

Katika wakati wake wa mapumziko, Dimmy anapendelea kuendesha gari, kushauriana na kampuni changa zinazoanza kwenye Go-To-Market (GTM) & mikakati ya mabadiliko ya Dijitali na kufanya kazi kwenye mradi wake wa PropTech.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live