Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

ATCL yazindua safari za Tanzania - Afrika Kusini

Video Archive
Fri, 28 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) leo Ijumaa Juni 28, 2019 limezindua rasmi safari za kutoka Tanzania kwenda Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Ndege ya ATCL aina ya Airbus 220-300 imeondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam Tanzania (JNIA)  saa 4:30 asubuhi ikitarajia kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa OR Tambo, Afrika Kusini saa 6:45 mchana.

Akizungumza na waandishi kabla ya ndege hiyo kuondoka leo Ijumaa, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa amesema lengo la kuanzishwa kwa safari hiyo ni kupunguza muda wa safari kwani abiria walikuwa wanaunganisha ndege ili kufika Afrika Kusini.

Kwandikwa amesema safari hii pia itasaidia kuboresha mahusiano ya kidiplomasia baini ya nchi hizi mbili.

"Tupo tayari kuhudumia Watanzania na tutaendelea kufungua safari nyingi duniani," amesema Kwandikwa

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, Emmanuel Koroso amesema Afrika Kusini ni maalumu kwa ajili ya biashara na utalii.

Pia Soma

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi amesema shirika hilo litafanya safari mara nne kwa wiki lengo ni kuwapa fursa Watanzania kupunguza muda wa safari badala ya kupitia Ethiopia au Nairobi- Kenya waweze kwenda moja kwa moja.

"Tunaomba Watanzania watupe ushirikiano na kupenda vya kwetu, tumeanza safari za kwenda Afrika Kusini na baadaye tunakwenda China na India," amesema

Kuhusu nauli, amesema zinauzwa kwa bei punguza ya Dola za Marekani 299 hadi Julai 15, 2019 kisha baada ya hapo bei mpya zitatangazwa.

Chanzo: mwananchi.co.tz