Watanzania Ibrahim Ramadhan na Fadi Ramadhan almaarufu Ramadhan Brothers, waliong'ara katika mashindano ya Australia’s Got Talent yaliyofanyika usiku wa Jumapili, Oktoba 16, 2022, wamefunguka mambo mengi kuhusu maisha yao ikiwemo jinsi walivyoanza sarakasi.
Watanzania Ibrahim Ramadhan na Fadi Ramadhan almaarufu Ramadhan Brothers, waliong'ara katika mashindano ya Australia’s Got Talent yaliyofanyika usiku wa Jumapili, Oktoba 16, 2022, wamefunguka mambo mengi kuhusu maisha yao ikiwemo jinsi walivyoanza sarakasi. Ramadhan Brothers wamesema shoo iliyoonekana kwenye mitandao na kuwapa umaarufu mkubwa pamoja na Golden Buzzers, ilikuwa ya utangulizi katika hatua za awali na kwamba zipo shoo nyingine kubwa zaidi ambazo Watanzania watajionea mambo makubwa waliyoyafanya wakiwa nchini Australia.