Kim Na-yoon, alipoteza mkono wa kushoto katika ajali ya pikipiki aliyoipata mwaka 2018. Ajali ambayo ilibadili mfumo wake mzima wa Maisha.
Alihisi ndoto yake ya kuwa katika ulimwengu wa uwanamitindo umegonga mwamba lakini hakupoteza matumaini maishani.
Alipokuwa akifanya mazoezi ya urekebishaji, alijipa changamoto ya kuwa mtaalamu wa kujenga misuli.
Kwa sasa anafanya vyema katika tasnia ya wanaojihusisha na utunishaji wa misuli katika maonesho mbali mbali Duniani.
Hivi karibuni aliibuka wa kwanza katika mashindano ya kujenga misuli, kuwashinda wanariadha wasio na ulemavu. Sasa anawasilisha ujumbe wake wa matumani kwa wengine.