Ndoto za kubeba taji la ligi ya kikapu ya Marekani (NBA) 2023-24 kwa nyota Giannis Antetokounmpo ( Milwaukee Bucks) na Joel Embiid (Philadelphia 76ers ) zimeota mbawa baada ya timu zao kutolewa kwenye michezo ya NBA Play-offs 2024 inayoendelea nchini Marekani.
Ndoto za kubeba taji la ligi ya kikapu ya Marekani (NBA) 2023-24 kwa nyota Giannis Antetokounmpo ( Milwaukee Bucks) na Joel Embiid (Philadelphia 76ers ) zimeota mbawa baada ya timu zao kutolewa kwenye michezo ya NBA Play-offs 2024 inayoendelea nchini Marekani. Joel Embiid ambaye ni mshindi wa tuzo ya Kia NBA MVP 2022-23 ameshuhudia timu yake ikitolewa leo kwa matokeo ya jumla ya 4-2 baada ya kufungwa na New York Knicks kwa alama 118-115 huku Giannis Antetokounmpo ambaye hajashiriki mchezo wowote wa Play-offs 2024 kwa jeraha la mguu,timu yake ya Milwaukee Bucks imeondoshwa na Indiana Pacers kwa jumla ya matokeo 4-2 baada ya kufungwa alama 120-98 na Indiana Pacers leo Alfajiri ya Mei 03-2024