Timu ya Pazi rasmi imetolewa kwenye mashindano ya kufuzu Ligi ya Mabingwa Afrika kwa upande wa mpira wa kikapu (BAL) yanayofanyika Afrika ya Kusini baada ya kupoteza michezo yote mitatu waliyocheza katika hatua ya makundi.
Pazi ilipoteza mchezo wa kwanza dhidi ya NBA Academy kwa pointi 57-84, wakapoteza dhidi ya Capetown Tigers pointi 87-95 na jana walipoteza mchezo wa mwisho dhidi ya Dynamo ya Burundi kwa pointi 85-88 na hivyo kushindwa kufuzu hatua ya nusu fainali.
Timu zilizofanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali kutoka kundi A ilipokuwa Pazi ni Daynamo ya Burundi na Capetown Tigers ya Afrika Kusini.