Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Mpira wa Kikapu

Mtoto wa LeBron James apata mshtuko wa moyo

Mtoto Wa LeBron James Apata Mshtuko Wa Moyo Mtoto wa LeBron James apata mshtuko wa moyo

Wed, 26 Jul 2023 Chanzo: Bbc

Bronny James, mtoto mkubwa wa mchezaji wa mpira wa kikapu LeBron James, yuko katika hali nzuri baada ya kupata mshituko wa moyo, msemaji wa familia hiyo amesema.

Taarifa ilisema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 alikuwa akifanya mazoezi na timu ya mpira wa kikapu ya Chuo Kikuu cha Southern California (USC) wakati tukio hilo lilipotokea.

"Wahudumu wa afya waliweza kumtibu Bronny na kumpeleka hospitali," ilisema taarifa hiyo.

"Kwa sasa yuko katika hali nzuri na hayuko tena ICU (kitengo cha wagonjwa mahututi)."

Iliongeza: "Tunaomba heshima na faragha kwa familia ya James na tutavifahamisha vyombo vya habari wakati kuna habari zaidi.

"LeBron na [mke wake] Savannah wanataka kutoa hadharani shukrani zao za dhati na shukrani kwa wagudumu wa matibabu na maafisa wa riadha kwa kazi yao nzuri na kujitolea kwa ajili ya kulinda usalama wa wanariadha wao."

Gwiji wa NBA Magic Johnson alisema "tunasali na tunatumaini atapona kwa haraka na haraka".

Chanzo: Bbc