Sat, 1 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uongozi unaosimamia Ligi ya Kikapu ya NBA umeboresha sera zake kuhusu matumizi ya bangi kwa kuiondoa katika kipengele cha madawa yanayozuiwa kwa wachezaji.
Hivyo, wachezaji wa NBA hawatafanyiwa vipimo kwa muda wa miaka saba kutokana na mkataba uliosainiwa na Collective Bargaining Agreement (CBA).
Mwaka 2022, nyota wa Timu ya Phoenix Suns, Kevin Durant alinukuliwa akiweka wazi kuwa alianza kuvuta bangi akiwa na umri wa miaka 22 na imemsaidia kuweka akili yake sawa na anapoitumia ni kama anakunywa mvinyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live