Nyota wa LA Lakers, Lebron James ndiye mchezaji pekee kwa sasa kushinda michezo mingi zaidi, michezo 41 ya NBA Playoffs na kumpiku Derek Fisher mchezaji wa zamani wa Lakers aliyekuwa anaishikilia rekodi hiyo.
Nyota wa LA Lakers, Lebron James ndiye mchezaji pekee kwa sasa kushinda michezo mingi zaidi, michezo 41 ya NBA Playoffs na kumpiku Derek Fisher mchezaji wa zamani wa Lakers aliyekuwa anaishikilia rekodi hiyo. Lebron ameiweka rekodi hiyo baada ya kufunga alama 30, rebound 9 na assist 9 zilizoisaidia timu yake ya Lakers kuibuka na ushindi wa alama 122-101 dhidi ya Golden State Warriors na Lakers kutinga fainali ya Ukanda wa Magharibi kwenye NBA playoffs asubuhi ya Leo Jumamosi Mei 13, 2023.