Tue, 23 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kuchapwa fagio na Denver Nuggets alfajiri ya leo na kushuhudia timu yake Los Angeles Lakers ikishindwa kuingia fainali ya NBA mwaka huu, LeBron James anafikiria kustaafu mchezo wa Kikapu.
Akiongea na waandishi baada ya mchezo, LeBron alimaliza mkutano huo kwa kusema “Kuendelea na mchezo wa Kikapu, nina mengi ya Kufikiria.”
Alienda mbali zaidi na kufafanua kauli hiyo akisema;
“Nitafikiria kama nitaendelea kucheza, hasa mwakani.” alisema James (38) ambaye amekamilisha misimu 20 ya NBA.
Una lipi la kusema kuhusu uamuzi huu wa LeBron James?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live