Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Mpira wa Kikapu

LeBron James aweka rekodi ya Dunia

LAKER LEBRONE LeBron James

Wed, 18 Jan 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Nyota LeBron James amefunga alama 48 zikiwa ni alama nyingi kwake kufunga kwa msimu huu na kuisaidia timu yake Los Angeles Lakers kuwalaza Houston Rockets kwa alama 140 dhidi ya alama 132 kwenye mchezo wa ligi ya kikapu ya Marekani (NBA).

LeBron mwenye miaka 38 sasa anafikisha alama 38,072 kwenye orodha ya ufungaji wa muda wote ndani NBA akiwa nyuma ya alama 315 za kinara wa ufungaji wa muda wote kwenye NBA Kareem Abdul-Jabbar.

Matokeo mengine,Boston Celtics imewalaza Charlotte Hornets kwa alama 130-118 huku nyota Jayson Tatum akifunga alama 51 kwa mara ya saba ndani ya msimu huu na kuchukua ribaundi 9 na kutoa pasi za usaidizi wa mabao mara 5 huku nyota Steph Curry ameisadia Golden State Warrior kuwalaza Washington Wizards kwa alama 127 dhidi ya 118 huku akifunga alama 41 na kuchukua ribaundi mara 7.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live