Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Mpira wa Kikapu

Kevin Durant anasema 'kila mtu hutumia' bangi katika NBA

Kevin Durant Anasema 'kila Mtu Hutumia' Bangi Katika NBA Kevin Durant anasema 'kila mtu hutumia' bangi katika NBA

Fri, 28 Jul 2023 Chanzo: Bbc

Nyota wa mpira wa vikapu Kevin Durant amesema kuwa kamishna wa NBA aliweza kunusa harufu ya bangi alipokuwa akishawishi – kumalizika kwa marufuku ya ligi dhidi ya bangi.

"Alinusa harufu nilipoingia ndani, kwa hivyo sikulazimika kusema mengi, unajua ninachosema?" Durant alisema katika mahojiano.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 aliongeza kuwa dawa hiyo inatumika sana kwenye ligi "ni kama mvinyo kwa wakati huu".

Wachezaji wa NBA hawaruhusiwi tena kutumia bangi.

Ligi hiyo na muungano wake, Chama cha Kitaifa cha Wachezaji wa Mpira wa Kikapu, walitia saini makubaliano mapya ya mazungumzo ya pamoja mwezi uliopita ambayo yataondoa dawa hiyo kwenye orodha yake ya dawa zilizopigwa marufuku.

Mabadiliko hayo ya sera yalileta sifa kutoka kwa rapper Snoop Dogg, ambaye alisifu "faida zake za kiafya na jinsi inavyoweza kusaidia kupunguza tembe zote ambazo wamepewa na sindano".

Wacheza hawajafanyiwa majaribio ya matumizi ya bangi tangu msimu wa ligi wa 2019-2020.

Durant, mshambuliaji wa Phoenix Suns na mmoja wa wafungaji bora katika historia ya NBA, alikuwa miongoni mwa wale ambao binafsi walimshawishi kamishna wa NBA Adam Silver katika mkutano wa kusimamisha ligi kama adhabu kwa matumizi ya dawa hiyo.

Chanzo: Bbc