Wed, 18 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa Timu ya Mpira wa Kikapu ya Golden State Warriors wanaoshiriki Ligi ya NBA wametembelea Ikulu ya Marekani (White House) na kukutana na Rais wa Marekani Joe Biden, jana Jumanne.
Warriors wameshinda mataji manne ya NBA ndani ya miaka 8 lakini hawakuwahi kutembelea White House kipindi Donald Trump ni Rais wa nchi hiyo.
Trump aliwahi kutamka hadharani kuwa hatawaalika Warriors kufuatia Steph Curry ambaye ni nyota wa timu hiyo, kusema hawezi kukanyaga sehemu hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live