Timu ya Kikapu ya Milwaukee Bucks inayoshiriki Ligi ya NBA (Eastern Conference) wamemuajiri Kocha wa zamani wa Los Angeles Clippers, Doc Rivers ili kuinoa timu hiyo kuchukua nafasi ya Adrian Griffin waliyeacha kufanya nae kazi
Milwaukee Bucks jukumu kubwa walilompa Kocha huyo mpya ni kuhakikisha anawapa Ubingwa wa Ligi hiyo kwani wanataka ubingwa wa pili ndani ya misimu minne (4) na mpaka sasa timu hiyo inashika nafasi ya pili (2) kwenye msimamo wa Eastern Conference nyuma ya Boston Celtics wakiwa na rekodi ya 30-13
Mara ya mwisho kwa Kocha Doc Rivers kuchukua ubingwa ni alivyokuwa na Boston Celtics mwaka 2008 na tangu aondoke Boston Celtics mwaka 2013 hajawahi kuchukua ubingwa wa NBA.