Tue, 26 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakongwe wa muziki TID na CHILLAH wamemchana Babalevo ambaye siku kadhaa zilizopita alifanya interview na kuwahasa wakongwe hao kutumia vizuri nafasi walioipata sasa kuelekea utambulisho wa nyimbo yao ya kwanza toka wapatane
TID na CHILLAH wanasema kuwa Baba Levo anabebwa na Wasafi na kuwa hajui kuimba anapiga kelele tu.
Lakini pia wawili hao wameshukuru kitendo cha Harmonize kuwapa nyota tano za Ufalme kupitia Instastory yake ambapo wamesema kuwa Harmonize anajua vipaji halisi na wanatamani ashiriki kwenye Album yao mpya wanayoiandaa
Chanzo: www.tanzaniaweb.live