Wed, 26 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
CEO wa Lebo ya WCB Diamond Platnumz ameweka wazi kufutika kwa material Ya Video Ya wimbo pendwa kwa sasa nchini "Enjoy" alioimba na Juma Jux.
Kutokana na janga hilo Diamond amesema wata-Shoot tena upya na itatoka Jumapili ya wiki hii.
Watu wengi walikuwa wakiisubiri kwa hamu Video ya wimbo huo ambao unafanya vyema katika Platform mbalimbali za muziki.
Je una lipi la kusema kwa Mondi na Jux? Tupia Comment yako
Chanzo: www.tanzaniaweb.live