Msanii wa Bongo Fleva, Ali Salehe Kiba, maarufu kama 'Alikiba' au 'King Kiba' amejinyakulia zaidi ya shilingi milioni tano kwenye hafla ya kugawa Mirabaha iliyofanyika Julai 21, 2023 Dar es Salaam.
Mirabaha hiyo imetolewa usiku wa jana Ijumaa Julai 21, 2021 na COSOTA na kuhudhuriwa na wasanii, viongozi na wadau mbalimbali wa sanaa katika hoteli ya Hayatt Regency jijini Dar es Salaam.
1. Diamond Platnumz - Sh7.7 milioni
2. Alikiba - Sh5.0 milioni
3. Rayvanny - Sh4.9 milioni
4. Zuchu - Sh4.7 milioni
5. Mbosso - Sh4.2 milioni
6. Nandy - Sh3.5 milioni
7. Harmonize - Sh3.4 milioni
8. Maua Sama - Sh2.3 milioni
9. Young Lunya - Sh1.7 milioni
10. G Nako - Sh1.3 milioni.