Wed, 16 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkimbiaji mmoja kutokea China ambaye ni maarufu kwa kukimbia huku akivuta sigara, majuzi aliimaliza marathon ya Xin'anjiang karibu na Shanghai katika muda ulioshangaza wengi.
Chen (50) anayejulikana zaidi kama "Uncle Chen" amekuwa maarufu kwa kukimbia mbio mbalimbali na kuzimaliza huku akivuta sigara muda wote.
Wiki iliyopita Uncle Chen alimaliza marathon ya kilomita 42 ndani ya masaa matatu na dakika 28 na kushika namba 574 kati ya wakimbiaji 1,500.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live