Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Zari kafunguka kuhusu wanaotumia jina lake kutapeli watu

58d0e03ac45a727a Zari The Boss Lady

Mon, 20 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Sosholaiti maarufu kutoka Uganda Zari Hassan amewatahadharisha mashabiki wake kuhusu matapeli ambao wamekuwa wakitumia majina na picha zake kuomba misaada ya kifedha.

Zari aliwashauri mashabiki wake kuepukana na watu wanaojifanya kuwa yeye mitandao ili kuomba msaada wa fedha.

Zari Hassan amewaonya mashabiki wake dhidi ya matapeli ambao wamekuwa wakitumia majina na picha zake kuomba misaada ya kifedhaKupitia mtandao wa Instagram, Zari alisema hujawahi omba msaada wowote kwa ajili ya kufanya kazi ya hisani.

Kupitia kwenye mtandao wa Instagram, mfanyabiashara huyo ambaye kwa sasa anaishi Afrika Kusini, alikana kwamba hajawahi omba msaada wowote wa kifedha kwa ajili ya kuendesha kazi yake ya uhisani.

Zari pia alikana madai kwamba anafanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni na ana miliki shirika ambalo huwasaidia watu kwenda ughaibuni.

" Sifanyi biashara ya kubadilisha fedha za kigeni,(forex), na sijawahi omba msaada wa kifedha kwa ajili ya kuendesha kazi yangu ya hisani, hakuna shirika kama Zari Foundation ambalo linafadhili vituo vya watoto yatima, tafadhili msikubali kulaghaiwa," Zari alisema.

" Mimi sina shirika wala kampuni ya kuwasaidia watu kwenda ughaibuni, nimeon kuna tangazo moja mitandaoni likiwa na picha yangu. Kuna watu wengi ambao wameibiwa lakini bado mimi hufahamishwa, hizo ni picha zangu zinatumika na matapeli, tafadhali epukana nao kabila, wazuie na upige ripoti," Aliongezea Zari.

Awali, mama huyo wa watoto watano alifichua kwamba hana mchumba kwa sasa na hana mpango wa kuingia tena kwenye uhusiano wa kimapenzi baada ya kuachana na mpenzi wake wa hivi punde.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke